Saturday, January 5, 2008

“Sisi ni wageni wa nani leo.”

A response to another blogger in kiswahili.
PHILIP OCHIENG has a nice take on the killing, "Attacking one's neighbour is misplaced anger.


Ubaya wetu haukuanza na kura tarehe 27, 2007, sisi kila siku tunaona binaadamu wenzetu wakidhulumiwa. Mara ngapi tumesimama na kuangalia kama hayawani mwizi akichomwa na tairi. Ndio wizi ni tabia mbaya, lakini tukifika pahali pakumchoma binaadamu mwenzetu, kwasababu ya shilingi kumi, basi huwa hatuna utu.

Ni jambo muhimu tujiulize, kwanini siku zilizopita hatukuwa na ushujaa na kusema sheria lazima ipewe nafasi, na tuhakikishe wale walio na jukumu hilo la kuhukumu wezi wa aina yeyote, wako na uwezo. Kama wakishindwa kufanya kazi yao, basi hao ndio maadui zetu na kama hatua itachukuliwa, sio huyo masikini mwenzako anafaa kutiwa tairi, bali hao askari, majaji, wana siasa, mawaziri mpaka rais mheshimiwa.

Ukabila upo na sio wakati wa kujadiliana kuhusu ubaguzi, bali tujiulize "utu wetu uko wapi leo." Aibu sio kwa huyu ama yule, Mkikuyu, Mjaluo , Mkalenjin ama Kibaki na Raila, dunia nzima inaona uchi wetu. Aibu ilioje leo. Elimu yetu yote haina faida wala utajiri wakupindukia.

Kanisa linatiwa moto na binaadamu, watoto na kina mama. Bado tunazungumza kama hiyo ni sawa. Muerevu ni yule atakubali kuwa sote tuko na makosa.

Umasikini wakupindukia unatuangalia asubuhi na jioni.
Watoto wa barabarani wanavuta gamu.
Barabara zimejaa mashimo kutoka Busia mpaka Mombasa.
Matajiri na magari ghali vijijini.
Mawaziri wana peleka nguo kufuliwa uingereza.
Ofisi gorofa ya pili, kabila moja.
Kupata kibali kwenda kuja kesho.
Hospitali ya serikali,daktari anauliza “wapi sindano yako.”
Jiji kuu la Nairobi limejaa takataka.
Haina haja kuendelea, hata kipofu atasema, "Harufu mbaya."
Mimi na wewe ndio tulitia moto Kanisani.
Waliokufa kifo kibaya chakusikitisha, sio Wakikuyu.
Tumewauwa ndugu zetu.
Nakuuliza, “sisi ni wageni wa nani leo.”

No comments:

Blog Archive

About Me

My photo
Kibaki must be held responsible for the bloodshed. ECK has no excuse, they too can be charged for complicity to commit genocide. Those who are looking at the tribal hatred and murder might be naive to try to blame Raila, but the truth is Kibaki number 2, must be stopped by any means necessary. The signs are very clear, "A Tribal Dictatorship." Kenyans had no problem in the last election when Kibaki, a Kikuyu ran against Uhuru, another Kikuyu. It is time for Kikuyus to stand up and smell the chai. Kikuyus are the poorest and the most oppressed. Shoot to Kill has always been used against Kikuyus "Del Monte." The only matatus that must go to the police station for a strip search, are the ones going to Kikuyuland. There are more Kikuyus in prison than any other group. Kikuyus just like they rejected Uhuru and what he stood for, can reject Kibaki for trying to bring back the KANU type dictatorship. Raila and Luos should also be very careful when making statements about the election. Kenyans did not vote for Raila the Luo; Kenyans voted for Raila the ODM nominee.