Sunday, December 30, 2007

Kibaki Kibaraka

Kama kweli Kibaki ana utu na kufahamu historia ya dhulma Kenya, basi angeondoka bila ya raia kudhulumiana. Hivi naandika na huku wanaKenya katika mitaa ya Kibera, Kisauni na kwengineko waumizana. Biashara na nyumba nyingi za raia zinawaka moto.

Kwa kweli kulingana na ushaidi kutoka kila pahali, dalili ni wizi usio na mfano wa kura umetokea. Kulingana na habari kutoka Meru, taa zilipotea kwa mda na zilipowaka, kura za Kibaki zilikuwa zimevimba. Basi sio haki kumuita rais mwizi, lakini hakuna shaka wengi watamkumbuka kwa jina baya.

Kwa ufupi Wakenya wamesema, Ukabila hauna pahali Kenya. Wakikuyu ni afadhali waitikie, wasimamae bila ya kuogopa, waseme wao ni wakenya na wanaheshimu sheria.

Kenya sio ya kabila hili ama lile
Kenya sio ya wakikuyu ama wajaluo
Kenya ya leo sio kama nchi zengine za udikteta
Wakikuyu hawana budi, bali kukubali
Kenya ni kubwa na bora kuliko nyumba ya Mumbi
Baba Raila akampa Kenyatta Mkikuyu urais
Mwana Odinga akamsaidia Kibaki, pia mkikuyu
Kumuonda dikteta Moi bila ya kumdhulumu
Basi ni wakati wakikuyu angaa wasimame kwa umoja
Waseme asante sana kwa kuturuhusu kutawala
Waseme kwa sauti kubwa na umoja, si lazima tutawale

Read more!

Blog Archive

About Me

My photo
Kibaki must be held responsible for the bloodshed. ECK has no excuse, they too can be charged for complicity to commit genocide. Those who are looking at the tribal hatred and murder might be naive to try to blame Raila, but the truth is Kibaki number 2, must be stopped by any means necessary. The signs are very clear, "A Tribal Dictatorship." Kenyans had no problem in the last election when Kibaki, a Kikuyu ran against Uhuru, another Kikuyu. It is time for Kikuyus to stand up and smell the chai. Kikuyus are the poorest and the most oppressed. Shoot to Kill has always been used against Kikuyus "Del Monte." The only matatus that must go to the police station for a strip search, are the ones going to Kikuyuland. There are more Kikuyus in prison than any other group. Kikuyus just like they rejected Uhuru and what he stood for, can reject Kibaki for trying to bring back the KANU type dictatorship. Raila and Luos should also be very careful when making statements about the election. Kenyans did not vote for Raila the Luo; Kenyans voted for Raila the ODM nominee.