Friday, January 4, 2008

Man Beaten To Death In Kenya( bado tumelala)

Habari Nyote, (Anaglia Kenya Yetu, hawa ni ndugu zetu)
Tafadhali soma.

Hapa Dayton tuko na wakikuyu na wajaluo wengi na makabila mengine kidogo, lakini sote ni wakenya. Najua kuna chuki baina ya wengi. Chuki ambayo haina msingi wakati ndugu zetu wanauana bure.

Natuma barua na picha kila wakati nikijua wengi wanasoma. Sababu kubwa ya kutuma ni kuhakikisha milango ya mawasiliano iko wazi. Jina langu ni Mohamed, ndio mimi ni Muislamu na wengi wenzangu ni Wakristo, lakini ukiuliza mtu yeyote ambaye ananifahamu, atacheka nakujibu, "huyo Mohamed Mkenya." Pia wewe na wengine, majirani wako wanakujua kama Mkenya.

Barua hii singeweza kuandika, isipokuwa tuko pahali pabaya sana wakenya wenzangu. Tusingojee mambo yaharibike kabisa na Kenya kubadilika iwe kama Somalia ama nchi zingine duniani ambazo ziko katika habari kila siku. Najua wengi hawataki Kenya izungumzwe vibaya. Tusimame kama binaadamu walio barikiwa, tufanye kazi ya haki.

Mungu ametuchagua kuwa pahali ambapo tunaweza kufanya makubwa. Tusaidie nci yetu na ndugu zetu. Basi nawaomba musimame tufanye kazi. Leteni maoni.

Kama kazi yako ni kusaidia wengine, simama uisabiwe
Kama wewe ni mwalimu, simama uisabiwe.
Kama wewe ni daktari, simama uisabiwe
Kama wewe ni fundi simama uisabiwe.
Kama wewe ni mwandishi, simama uisabiwe.
Kama wewe ni mwanafunzi, simama uisabiwe.
Kama wewe ni tajiri, simama uisabiwe.
Kama wewe ni masikini, simama uisabiwe.
Kama wewe ni muhubiri, simama uisabiwe.
Kama wewe ni Mkenya, LAZIMA usimame uisabiwe.
MVUKA itasimama iisabiwe. Huu ndio wakati wakutumia MVUKA.
Mola ametubariki na viongozi wazuri walio hakikisha,
"Miami Valley United Kenya Association," iko hai.

Asanteni sana na Mola awabariki,

Mohamed Ahmed
aka: Kamau Onyango

No comments:

Blog Archive

About Me

My photo
Kibaki must be held responsible for the bloodshed. ECK has no excuse, they too can be charged for complicity to commit genocide. Those who are looking at the tribal hatred and murder might be naive to try to blame Raila, but the truth is Kibaki number 2, must be stopped by any means necessary. The signs are very clear, "A Tribal Dictatorship." Kenyans had no problem in the last election when Kibaki, a Kikuyu ran against Uhuru, another Kikuyu. It is time for Kikuyus to stand up and smell the chai. Kikuyus are the poorest and the most oppressed. Shoot to Kill has always been used against Kikuyus "Del Monte." The only matatus that must go to the police station for a strip search, are the ones going to Kikuyuland. There are more Kikuyus in prison than any other group. Kikuyus just like they rejected Uhuru and what he stood for, can reject Kibaki for trying to bring back the KANU type dictatorship. Raila and Luos should also be very careful when making statements about the election. Kenyans did not vote for Raila the Luo; Kenyans voted for Raila the ODM nominee.